Kituo: Selian Agricultural Research Institute - Arusha
Mbegu: Selian H215
Sifa za mbegu
- Aina hii ni mahindi chotara.
- Inastawi katika mwinuko wa mita 800 hadi 1,200 kutoka usawa wa bahari.
- Inakomaa kati ya siku 105 hadi 148.
- Inatoa mavuno ya wastani wa tani 5 kwa hekta.
- Inastahimili ugonjwa wa bakajani kijivu wa mahindi (grey leaf spot) hususan katika maeneo ya kanda ya kaskazini.
Kituo: Kituo Cha Utafiti Ilonga – Kilosa Morogoro
Mbegu: 1. WE4106
Sifa za mbegu
- Aina hii ni mahindi chotara.
- Inastawi katika ukanda wa chini na kati wa mita 0 hadi 1,500 kutoka usawa wa bahari.
- Inakomaa kwa wastani wa siku 106.
- Ina ukinzani wa magonjwa ya milia ya mahindi (maize streak), bakajani kijivu wa mahindi (grey leaf spot) na kutu ya majani (leaf rust).
- Inakoboleka vizuri (good poundability).
- Inatoa mavuno ya wastani wa tani 6.8 kwa hekta.
- Inastahimili ukame.
2. WE4102
Sifa za mbegu
- Aina hii ni mahindi chotara.
- Inastawi katika ukanda wa chini na kati wa mita 0 hadi 1,500 kutoka usawa wa bahari.
- Inakomaa kwa wastani wa siku 105.
- Ina ukinzani wa magonjwa ya milia ya mahindi (maize streak), bakajani kijivu wa mahindi (grey leaf spot) na kutu ya majani (leaf rust).
- Inakoboleka vizuri (good poundability).
- Inatoa mavuno ya wastani wa tani 6.7 kwa hekta.
- Inastahimili ukame.
3. WE4110
Sifa za mbegu
- Aina hii ni mahindi chotara.
- Inastawi katika ukanda wa chini na kati wa mita 0 hadi 1,500 kutoka usawa wa bahari.
- Inakomaa kwa wastani wa siku 101 hadi 111.
- Ina ukinzani wa magonjwa ya milia ya mahindi (maize streak), bakajani kijivu
- wa majani (grey leaf spot) na kutu ya majani (leaf rust).
- Inakoboleka vizuri (good poundability)
- Inatoa mavuno ya wastani wa tani 6.6 kwa hekta.
- Inastahimili ukame.
4. WE4114
Sifa za mbegu
- Aina hii ni mahindi chotara.
- Inastawi katika ukanda wa chini na kati wa mita 0 hadi 1,500 kutoka usawa wa bahari.
- Inakomaa kwa wastani wa siku 102.
- Ina ukinzani wa magonjwa ya milia ya mahindi (maize streak), bakajani kijivu wa mahindi (grey leaf spot) na kutu ya majani (leaf rust).
- Inakoboleka vizuri (good poundability).
- Inatoa mavuno ya wastani wa tani 5.9 kwa hekta.
- Inastahimili ukame.
4. WE4115
Sifa za mbegu
- Aina hii ni mahindi chotara.
- Inastawi katika ukanda wa chini na kati wa mita 0 hadi 1,500 kutoka usawa wa bahari.
- Inakomaa kwa wastani wa siku 104 hadi 112.
- Ina ukinzani wa magonjwa ya milia ya mahindi (maize streak), bakajani kijivu wa mahindi (grey leaf spot) na kutu ya majani (leaf rust).
- Inakoboleka vizuri (good poundability).
- Inatoa mavuno ya wastani wa tani 6.4 kwa hekta.
- Inastahimili ukame.
5. WE4112
Sifa za mbegu
- Aina hii ni mahindi chotara.
- Inastawi katika ukanda wa chini na kati wa mita 0 hadi 1,500 kutoka usawa wa bahari.
- Inakomaa kwa wastani wa siku 103.
- Ina ukinzani wa magonjwa ya milia ya mahindi (maize streak), Ukungu kijivu wa mahindi (grey Leaf spot) na kutu ya majani (leaf rust).
- Inakoboleka vizuri (good poundability)
- Inatoa mavuno ya wastani wa tani 6.5 kwa hekta.
- Inastahimili ukame.
Kituo: Kituo Cha Utafiti Tumbi - Kibaha
Mbegu: 1. T104
Sifa za mbegu
- Aina hii ni mahindi ya kawaida (OPV)
- Inastawi katika ukanda wa kati katika mwinuko wa mita 600 hadi 1,500.
- Inakomaa kwa wastani wa siku 104 hadi 128.
- Inatoa mavuno ya wastani wa tani 4.5 kwa hekta.
2. T105
Sifa za mbegu
- Aina hii ni mahindi ya kawaida (OPV)
- Inastawi katika ukanda wa kati katika mwinuko wa mita 600 hadi 1500.
- Inakomaa kwa wastani wa siku 103 hadi 129.
- Inatoa mavuno ya wastani wa tani 5.4 kwa hekta.
Kituo: Aminata Quality Seeds & Consultancy Ltd - Tanga
Mbegu: 1. NATA H401
Sifa za mbegu
- Aina hii ni mahindi chotara.
- Inastawi katika ukanda wa chini na kati katika mwinuko wa mita 400 hadi 1,500.
- Inakomaa kwa wastani wa siku 120 hadi 130.
- Inatoa mavuno ya wastani wa tani 7 kwa hekta.
- Inastahimili ugonjwa wa bakajani kijivu wa mahindi (grey leaf spot), baka jani (leaf blight) na kutu ya majani (leaf rust).
- Inakoboleka vizuri (good poundability).
2. NATA K 8
Sifa za mbegu
- Aina hii ni mahindi ya kawaida (OPV).
- Inastawi katika ukanda wa chini na kati katika mwinuko wa mita 0 hadi 1,600.
- Inakomaa kwa wastani wa siku 110 hadi 120.
- Inastahimili magonjwa ya bakajani wa mahindi (grey leaf spot), milia (maize streak virus) na ‘Turcicum blight’.
- Inatoa mavuno ya wastani wa tani 4.9
Kituo: Krishna Seed Company Ltd – Babati Manyara
Mbegu: 1. Krishna Hybrid-1
Sifa za mbegu
- Aina hii ni mahindi chotara.
- Inastawi katika mwinuko wa mita 600 hadi 1,200 kutoka usawa wa bahari.
- Inakomaa kwa muda wa siku 128.
- Inatoa mavuno ya wastani wa tani 6.9 kwa hekta.
- Inastahimili magonjwa ya majani wa ukungu kijivu wa mahindi (grey leaf spot) milia ya mahindi (maize streak virus).
2. Krishna Hybrid-2
Sifa za mbegu
- Aina hii ni mahindi chotara.
- Inastawi katika mwinuko wa mita 600 hadi 1,200 kutoka usawa wa bahari.
- Inakomaa kwa muda wa siku 134.
- Inatoa mavuno ya wastani wa tani 7.6 kwa hekta.
- Inastahimili magonjwa ya ukungu kijivu wa mahindi (grey leaf spot) na milia ya mahindi (maize streak virus).
Kituo: Meru Agro- Tours & Consultancy Co. Ltd – Arusha
Mbegu: 1. MERU LISHE 503
Sifa za mbegu
- Aina hii ni mahindi ya kawaida (OPV).
- Aina ya mahindi lishe yaliyo na kiwango kikubwa cha viini muhimu vya protini.
- Hustawi katika mwinuko wa mita 800-1,200 kutoka usawa wa bahari.
- Inakomaa mapema kwa wastani wa siku 99.
- Ina stahimili magonjwa ya bakajani kijivu wa mahindi(grey leaf spot)na milia ya mahindi ( maize streak virus).
- Inatoa mavuno ya wastani wa tani 4.3 kwa hekta.
- Inakoboleka kirahisi.
2. MERU LISHE 511
Sifa za mbegu
- Aina hii ni mahindi ya kawaida (OPV).
- Aina ya mahindi lishe yaliyo na kiwango kikubwa cha viini muhimu vya protini.
- Hustawi katika mwinuko wa mita 800-1,200 kutoka usawa wa bahari.
- Inakomaa kwa muda wa wastani wa siku 98.
- Ina ukinzani wa magonjwa ya bakajani kijivu wa mahindi (grey leaf spot) na milia ya mahindi (maize streak virus).
- Inatoa mavuno ya wastani wa tani 5.2 kwa hekta.
- Inakoboleka kirahisi.
Kituo: Iffa Seed Company Ltd - Arusha
Mbegu: 1. Kaspidi hybrid
Sifa za mbegu
- Aina hii ni mahindi chotara.
- Hustawi katika mwinuko wa mita 600 hadi 1,200 kutoka usawa wa bahari.
- Inakomaa kwa muda wa siku 150 hadi siku 155.
- Inatoa mavuno ya wastani wa tani 6.1 kwa hekta.
- Inastahimili magonjwa wa bakajani kijivu wa mahindi (grey leaf spot) na milia ya mahindi (maize streak virus).
2. Kisongo hybrid
Sifa za mbegu
- Aina hii ni mahindi chotara.
- Hustawi katika ukanda wa mwinuko wa mita 600 had 1,200 kutoka usawa wa bahari.
- Inakomaa katika siku 138.
- Inatoa mavuno ya wastani wa tani 6.8 kwa hekta.
- Inastahimili magonjwa ya bakajani kijivu wa mahindi (grey leaf spot) na milia ya mahindi (maize streak virus).
No comments:
Post a Comment